Ziara ya utalii katika Mkoa wa Alexandria ikiwa ni sehemu ya shughuli za siku ya tisa za toleo la tano la Udhamini wa Nasser

Jukwaa la Nasser la Kimataifa lilitangaza kupitia taarifa yake kuwa litaandaa ziara katika Mkoa wa Alexandria, ikiwa ni sehemu ya shughuli za siku ya tisa za toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa , unaofanyika katika mwezi huu wa Mei chini ya kaulimbiu “Misri na Umoja wa Mataifa: Miaka 80 ya  Uwakilishi wa Masuala ya Ulimwenguni Kusini”, kwa Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, na kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa, likiwakutanisha vijana takriban 150  wavulana na wasichana kutoka mataifa mbalimbali duniani, wakiwa ni viongozi vijana kutoka nyanja mbalimbali za kiutendaji, pamoja na vijana wenye ushawishi mkubwa katika jamii zao.

Jukwaa la Nasser la Kimataifa lilieleza kuwa ujumbe wa vijana wanaoshiriki katika toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, waliambatana katika ziara hiyo ya Alexandria na viongozi kadhaa, akiwemo Meja Jenerali Ismail El-Far, Msaidizi Mkuu wa Waziri wa Vijana na Michezo wa Masuala ya Vijana na Mahusiano ya Serikali; Bw. Alaa Desouki, Naibu Waziri na Mkuu wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Vijana; na Bw. Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Jukwaa la Nasser la Kimataifa na Mkurugenzi wa Ofisi ya Vijana wa Kusini ya Dunia.

Katika taarifa ya Jukwaa la Nasser la Kimataifa, ilielezwa kuwa ziara ya wajumbe wa vijana wanaoshiriki katika toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa katika Mkoa wa Alexandria ilijumuisha kutembelea Maktaba ya Alexandria, "taa ya maarifa na alama ya utamaduni."
Daktari Marwa El-Wakeely, Mkuu wa Idara ya Utafiti wa Kitaaluma katika maktaba hiyo, aliwapokea na kuwakaribisha vijana hao huku akiwapasha salamu kutoka kwa Dkt. Ahmed Zayed, Mkurugenzi wa Maktaba, Akisisitiza kuwa Maktaba ya Alexandria ni dirisha la Misri kwa dunia na taasisi mashuhuri ya kisayansi na kitamaduni katika ngazi ya kimataifa. Washiriki wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi walitembelea maktaba hiyo na kujifunza kuhusu historia ya kuanzishwa kwake, muundo wake wa kipekee ulio katika umbo la “kisahani cha jua,” pamoja na urithi wake wa kiutamaduni unaowakilisha tamaduni mbalimbali za dunia, jambo lililoifanya kuwa moja ya alama muhimu za maarifa na utamaduni katika ngazi ya kikanda na kimataifa. Pia, washiriki walitembelea sehemu mbalimbali za maktaba hiyo na kutazama kazi za sanaa za uchoraji na uchongaji zilizoko kwenye kuta zake, zinazoakisi historia ya Misri ya zamani, amani ya kijamii, uvumilivu wa kidini, pamoja na taswira za misikiti na makanisa maarufu ya Kimisri. Vilevile, walifahamishwa kuhusu tovuti rasmi ya maktaba na huduma zake za kidijitali zinazowezesha watu kunufaika nazo kwa njia ya mtandao. Katika muendelezo wa ziara yao ndani ya Maktaba ya Alexandria, wajumbe wa vijana waliotoka nchi mbalimbali pia walitembelea makumbusho kadhaa, ikiwemo: Makumbusho ya Hati na Vitabu Adimu, Makumbusho ya Mambo ya Kale, Maonesho ya “Alexandria katika Historia” (mikusanyiko ya Dkt. Mohamed Awad), na Ukumbi wa Shadi Abdel Salam.

Katika hitimisho la taarifa yake, Jukwaa la Kimataifa la Nasser lilieleza kuwa ziara hiyo ilikamilika kwa kuandaliwa kwa matembezi ya utalii ya kujitegemea kwa washiriki wa toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa katika Jiji la Alexandria. Washiriki walieleza furaha yao kubwa kwa kutembelea Mkoa wa Alexandria, maarufu kama Bibi Harusi wa Bahari ya Mediterania, na kuona vivutio vyake muhimu, sambamba na kufurahia hali yake ya hewa ya kuvutia. Pia walionesha furaha yao kwa kutembelea Maktaba ya Alexandria – taa ya maarifa – wakisisitiza kuwa wanathamini sana Misri, watu wake, historia yake adhimu na utofauti wa urithi wake wa ustaarabu. Washiriki wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi walituma ujumbe kupitia kurasa zao binafsi katika mitandao ya kijamii wakieleza furaha yao kwa ziara hiyo, na walipiga picha nyingi pamoja na kurekodi video wakati wa mwisho wa ziara yao katika maktaba, wakiwa katika hali ya furaha na msisimko mkubwa kwa fursa hiyo ya kipekee.

Kwa upande wake, Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Jukwaa la Nasser la Kimataifa, alisema kuwa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi unalenga kuwafahamisha vijana wa kimataifa wanaoshiriki katika Udhamini huu kuhusu alama za ustaarabu wa Misri na juhudi za uongozi wa kisiasa katika kufanikisha maendeleo makubwa katika sekta na nyanja mbalimbali. Hili linaonekana wazi kupitia ziara za washiriki katika Makao Makuu ya Serikali kwenye Mji Mkuu wa Utawala Mpya, Baraza la Seneti ya Misri, Kituo cha Mageuzi na Urekebishaji cha 10 Ramadan, Makumbusho ya Jeshi la Anga, na Maktaba ya Alexandria, sambamba na maeneo mengine yanayotarajiwa kutembelewa katika siku zijazo za Udhamini huu, yakiwemo Chuo cha Polisi cha Misri.

Ni vyema kutajwa kuwa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi ni jukwaa la kipekee kwa ajili ya kuwaandaa viongozi vijana wapya katika ngazi za kikanda na kimataifa. Toleo la tano la Udhamini huu linakuja kama sehemu ya dhamira ya kudumu ya Misri katika kusaidia masuala ya nchi za Kusini mwa dunia, kuimarisha mazungumzo baina ya tamaduni mbalimbali, pamoja na kuhamasisha uhamishaji wa maarifa ya maendeleo na uzoefu bora katika uongozi, usimamizi na kazi za kijamii.

Inayohusiana na mada hii: