“Ujumbe wa Vijana” washiriki wa awamu ya tano ya Mradi wa Uongozi wa Kimataifa wa Nasser watembelea Mamlaka ya Mfereji wa Suez

Chini ya Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri ya Misri, na kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa:

Jukwaa la Nasser la Kimataifa: “Ujumbe wa Vijana” washiriki wa awamu ya tano ya Mradi wa Uongozi wa Kimataifa wa Nasser watembelea Mamlaka ya Mfereji wa Suez

Jukwaa la Nasser la Kimataifa limetangaza katika taarifa yake kuwa limeandaa ziara kwa ajili ya washiriki wa toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa  katika Mamlaka ya Mfereji wa Suez, mkoani Ismailia, kama sehemu ya shughuli za siku ya kumi na mbili ya Udhamini huo, chini ya Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri ya Misri, na kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa, huku likihusisha takriban vijana 150 wa kiume na wa kike kutoka mataifa mbalimbali duniani, wakiwa ni viongozi chipukizi wa sekta mbalimbali za kiutendaji, pamoja na baadhi ya vijana wenye ushawishi mkubwa na mchango chanya katika jamii zao.

Ujumbe wa vijana walipokelewa na Khaled Taha, Mkuu wa Mahusiano ya Umma katika Mamlaka ya Mfereji wa Suez, kwa uwepo wa Reda Safina, Mkurugenzi Mkuu wa Programu za Kujitolea na Skauti, Dkt. Ihab Salah, Mkurugenzi wa Idara ya Vijana na Michezo mkoani Ismailia, Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Jukwaa la Nasser la Kimataifa na Mkurugenzi wa Ofisi ya Vijana wa Kusini Ulimwenguni, pamoja na viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Vijana na Michezo na Mamlaka ya Mfereji wa Suez.

Washiriki wa toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa walifanya ziara maalumu katika mkoa wa Ismailia, ambapo walianza kwa kutembelea handaki la Ismailia ni mojawapo ya mafanikio makubwa ya kihandisi katika historia ya kisasa ya Misri. Baada ya hapo, walielekea katika Kituo cha Uigaji na Mafunzo ya Baharini cha Mamlaka ya Mfereji wa Suez, ambako walipata fursa ya kushuhudia wasilisho la kina kuhusu Mfereji wa Suez, likijumuisha historia yake, hatua za maendeleo zilizofikiwa, na nafasi yake muhimu katika uendeshaji wa biashara ya kimataifa. Vilevile, walihudhuria wasilisho lingine lililotoa maelezo ya kina kuhusu Mfereji Mpya wa Suez, yaliyokuwa yakiambatana na takwimu rasmi na za kulinganisha kati ya hali ya uongozaji wa meli kabla na baada ya utekelezaji wa mradi huo. Wasilisho hilo lilieleza faida kuu za kiusalama na kiufundi zilizopatikana kutokana na mradi huo mkubwa, ikiwemo kuongezeka kwa usalama wa meli, uwezo wa mfereji kukabiliana na dharura, kupandishwa kwa hadhi ya kimataifa ya mfereji, pamoja na uwezo wa kupokea meli kubwa zaidi zenye miundo mikubwa na mizigo mizito. Pia ilisisitizwa jinsi mradi huo unavyochangia kwa kiasi kikubwa katika uchumi wa Misri na kuunga mkono miradi mikubwa ya kitaifa.

Katika ziara hiyo, washiriki pia walitazama filamu ya kihistoria iliyoonesha picha halisi za ushiriki wa wananchi wa Misri katika kununua hati za uwekezaji za Mfereji wa Suez, ikiwa ni ishara ya imani yao kwa mradi huu wa kitaifa na kwa uongozi wa kisiasa unaoongozwa na Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi. Viongozi wa vijana walifahamishwa pia kuhusu tukio la kihistoria la kuondoa meli ya mizigo ya Panama iliyokuwa imekwama, ambapo ilielezwa jinsi Mamlaka ya Mfereji wa Suez ilivyoshughulikia tukio hilo kwa ustadi mkubwa, na kuwa mfano wa mafanikio ya kitaifa katika kukabiliana na changamoto za kimataifa. Ziara hiyo ilihitimishwa kwa safari ya baharini ndani ya Mfereji Mpya wa Suez, ambapo washiriki walipata nafasi ya kujionea mafanikio hayo kwa macho yao, wakishuhudia kwa karibu dhamira ya Misri katika kuendeleza miundombinu kama sehemu ya msingi ya kufanikisha maendeleo endelevu.

Viongozi wa toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa kutoka Wizara ya Vijana na Michezo walitoa shukrani na pongezi zao kwa Mamlaka ya Mfereji wa Suez kwa kuwapokea na kuwahudumia wajumbe wa kimataifa wa vijana walioshiriki katika mradi huo, pamoja na kuwapa fursa ya kutembelea moja ya miundombinu muhimu zaidi ya meli duniani. Ziara hii imekuwa sehemu muhimu ya shughuli za mradi, inayoonesha ushirikiano wenye mafanikio kati ya Wizara ya Vijana na Michezo na Mamlaka ya Mfereji wa Suez.

Lengo la ziara hiyo lilikuwa kuwapa washiriki uelewa wa kina kuhusu maendeleo yanayoendelea katika eneo la Mfereji wa Suez na juhudi kubwa zinazofanywa na mamlaka, hasa kuhusu Mradi wa Mfereji Mpya wa Suez uliotekelezwa kwa muda wa mwaka mmoja tu kwa juhudi za wazawa wa Misri. Pia walielezwa kuhusu mafanikio ya mamlaka katika kukabiliana na changamoto kubwa kama vile ajali ya meli ya mizigo ya Panama, iliyidhihirisha ari, ujasiri, na uwezo wa Misri kukabili matatizo ya kiwango cha kimataifa. Ziara hiyo ilipokelewa kwa furaha na shukrani kubwa na washiriki wa mradi, kwani iliwapa picha halisi na ya kuvutia kuhusu uwezo wa kiufundi na wa kibinadamu wa Misri. Washiriki walionesha kuvutiwa kwao na nafasi ya kimkakati ya Mfereji wa Suez katika kusaidia uchumi wa dunia na kurahisisha biashara ya kimataifa.

Mbali na maarifa mapya waliyojipatia kuhusu maendeleo endelevu, washiriki walipata pia fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu kuhusu mbinu bora za maendeleo, hatua iliyochangia kuimarisha ushirikiano wa kimataifa kati ya vijana wa mataifa mbalimbali. Tukio hili lilidhihirisha nafasi muhimu ya Misri kama jukwaa la mazungumzo ya kimataifa kati ya viongozi vijana, na kuthibitisha hadhi yake kama taifa kiongozi katika kushughulikia masuala ya dunia.

Washiriki wa toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa walieleza furaha yao kubwa kutokana na uzoefu wa kipekee na wa kuhamasisha walioupata wakati wa ziara yao ya Mfereji wa Suez, mojawapo ya miundombinu muhimu ya usafirishaji duniani. Walisema kuwa ziara hiyo imejaa msukumo na imani mpya kuhusu uwezo wa taifa la Misri katika kutekeleza miradi mikubwa kwa muda mfupi kwa kutumia wataalamu na wafanyakazi wa ndani. Walisifu sana Mradi wa Mfereji Mpya wa Suez, uliotekelezwa kwa muda wa mwaka mmoja tu kwa mikono ya Wamisri, wakitamani mafanikio na ustawi wa kuendelea kwa juhudi za kuboresha njia hii muhimu ya usafiri wa kimataifa. Aidha, walimshukuru kwa dhati Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi kwa msaada wake kwa mradi huu wa kipekee wa uongozi, ambao umeongeza maarifa yao, na kuwawezesha kuunda urafiki mpya na vijana kutoka mataifa mbalimbali duniani. Kwa kuonesha furaha yao, washiriki walijitahidi kuhifadhi kumbukumbu ya tukio hilo kupitia picha za pamoja na video, ambazo watadumisha kama mojawapo ya sehemu za kukumbukwa zaidi katika safari yao ya kielimu na kijamii kupitia mradi huu.

Katika hitimisho la ziara yao mkoani Ismailia, washiriki walitembelea Kambi ya Al-Qursh, mojawapo ya miradi ya kisasa inayounga mkono miundombinu ya michezo katika mkoa huo. Katika ziara hiyo, walipata fursa ya kutembelea uwanja wa mpira wa miguu wenye viwango vya kimataifa ulio na viti vya watazamaji na vyumba vya kubadilishia nguo, uwanja wa mpira wa miguu wa wachezaji watano (5-a-side), uwanja wa mchezo wa padel, pamoja na kituo cha kuogelea chenye bwawa la nusu Olimpiki na bwawa la watoto. Zaidi ya hayo, walitembelea ukumbi wa mikutano wenye uwezo wa watu 250, jengo la utawala, sehemu za michezo ya mezani kama tenisi na biliadi, karakana za sanaa, jengo la mazoezi ya viungo, pamoja na majengo ya malazi yaliyojengwa kwa kiwango cha kisasa. Kambi hiyo inachukua eneo la mita za mraba 39,000 sawa na ekari tisa, na inawakilisha uwekezaji mkubwa wa serikali ya Misri katika kuendeleza vipaji na ustawi wa vijana. Washiriki walionesha kuvutiwa na hatua hizi za maendeleo, wakitambua juhudi za Misri katika kuwekeza kwa vijana na kujenga mazingira bora kwa maendeleo endelevu na ushirikiano wa kimataifa.

Inayohusiana na mada hii: