البحث

Vijana wa Udhamini wa Nasser kwa ziara ya kihistoria katika Piramidi za Giza

2025/05/25

Jukwaa la Nasser la Kimataifa limetangaza katika taarifa yake kuwa limeandaa ziara ya kihistoria katika eneo la Piramidi za Giza kwa ajili ya washiriki wa toleo la tano la Mfuko wa Kimataifa wa Uongozi wa Gamal Abdel Nasser. Ziara hiyo ilifanyika wakati wa ufunguzi wa siku ya kumi na tano ya Udhamini huo, unaoandaliwa chini ya Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, na kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa, ukihusisha takribani vijana 150 wa kike na kiume kutoka mataifa mbalimbali duniani, wakiwa ni viongozi chipukizi na wabunifu katika nyanja mbalimbali za kiutendaji, pamoja na vijana wenye ushawishi mkubwa katika jamii zao.

Ziara hiyo ya kihistoria iliwahusisha washiriki wa Udhamini wa  Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa – toleo la tano, ambapo walitembelea Piramidi za Giza – mojawapo ya maajabu saba ya dunia ya kale. Walijionea kwa karibu Sanamu ya Sphinx inayiakisi ubunifu mkubwa wa Wamisri wa kale katika sanaa ya uchongaji na tafsiri ya alama za kifalsafa. Ziara hiyo pia ilihusisha eneo la Panoroma linalotoa mwonekano mpana wa mandhari ya kihistoria, ambapo washiriki walipiga picha za kumbukumbu kwa ajili ya kuhifadhi nyakati hizi muhimu za kihistoria.

Wakati wa ziara yao katika eneo la piramidi, washiriki wa Udhamini wa Nasser walipata maelezo ya kina kutoka kwa waongozaji wa kitalii waliobobea kuhusu historia ya piramidi, siri za ujenzi wake, na mbinu za kisasa za usanifu majengo zilizotumiwa na Wamisri wa kale. Pia waliangaziwa kuhusu umuhimu wa kipindi hiki katika historia ya kifarao, hasa kuhusu maendeleo ya kisayansi, kifikra na kidini. Washiriki wengi walieleza mshangao wao na kuvutiwa kwao na ustaarabu wa kale wa Wamisri, ambao bado unaendelea kuvutia dunia licha ya kupita kwa maelfu ya miaka.

Ziara hiyo ilihitimishwa kwa kutembelea Sanamu ya Sphinx – mojawapo ya alama maarufu za kihistoria duniani, ambapo washiriki walipata fursa ya kutafakari kuhusu maumbo na maana ya sanamu hiyo kubwa, pamoja na kupiga picha wakiwa karibu nayo. Aidha, walinunua zawadi mbalimbali na nakala za kihistoria kama kumbukumbu ya tukio hili muhimu linaloonesha uhalisia na utajiri wa ustaarabu wa kale wa Misri.

Washiriki wa toleo la tano la Udhamini wa  Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa walieleza furaha yao kubwa kufuatia yale waliyoyaona miongoni mwa hazina za kihistoria zinazoonesha ukubwa na utukufu wa ustaarabu wa kale wa Misri. Walivutiwa na uimara wa majengo na usahihi wa usanifu wake, jambo linalodhihirisha ubunifu mkubwa wa Wamisri wa kale. Viongozi hawa chipukizi pia walieleza shukrani zao za dhati kwa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi kwa mageuzi makubwa ya kihistoria na kimaendeleo yanayoendelea kushuhudiwa nchini Misri, ambapo urithi wa kale unakutana na maendeleo ya kisasa. Vilevile, walimshukuru Waziri wa Vijana na Michezo, Dkt. Ashraf Sobhy, kwa kuwezesha fursa hii adhimu ya kujifunza kuhusu urithi wa kihistoria wa Misri na maendeleo ya kisasa ya ujenzi yanayodhihirika nchini humo.

Aidha, wajumbe wa mfuko huo walieleza kuvutiwa kwao na juhudi za serikali ya Misri katika kuandaa na kuendesha matukio ya kimataifa, wakisisitiza kwamba hatua hii inaonesha nafasi ya Misri kama mwenyeji wa majukwaa ya kimataifa ya vijana.
Kwa upande wao, washiriki waliandika machapisho kupitia kurasa zao binafsi kwenye mitandao ya kijamii, wakieleza kwa furaha na shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, kwa kujitolea kwake daima katika kudhamini na kuendesha matukio ya kimataifa yanayolenga kuwawezesha vijana na kuimarisha nafasi yao katika maendeleo endelevu. Viongozi hao wa vijana walisisitiza kuwa juhudi na msukumo wa Rais katika kushughulikia masuala ya vijana ndani na nje ya Misri ni ushahidi wa imani ya taifa la Misri katika uwezo wa vijana kama nguvu kuu ya kupeleka mbele maendeleo ya dunia ya kesho.

"Jukwaa la Nasser la Kimataifa": Ziara ya Kihistoria Katika Eneo la Majengo ya Kidini, Siku ya Kumi na Tano ya Udhamini wa  Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa  – Toleo la Tano

Jukwaa la Nasser la Kimataifa limetangaza kupitia taarifa yake kuwa ilifanyika pia ziara maalumu katika Eneo la Majengo ya Kidini lililopo Misri ya Kale, ikiwa ni sehemu ya shughuli za siku ya kumi na tano za toleo la tano la Mfuko wa Kimataifa wa Uongozi wa Gamal Abdel Nasser. Ziara hiyo iliwajumuisha vijana viongozi kutoka mataifa mbalimbali wanaoshiriki katika mfuko huo wa kimataifa.

Eneo la Majengo ya Kidini ni mojawapo ya maeneo ya kipekee yanayoakisi urithi wa kiustaarabu, kihistoria na kiutamaduni. Ni sehemu ambapo mipaka ya wakati na nafasi huonekana kuyeyuka, na ambapo dini kuu tatu za mbinguni — Uyahudi, Ukristo na Uislamu — huishi kwa amani na maelewano. Miongoni mwa vivutio vya eneo hilo ni Msikiti wa Amr Ibn Al-As, msikiti wa kwanza kujengwa nchini Misri na barani Afrika, na wa nne kwa ujumla katika historia ya Uislamu baada ya misikiti ya Madina, Basra na Kufa. Karibu na msikiti huo yapo makanisa na nyumba za watawa zilizobarikiwa na kupitiwa na Bwana Yesu Kristo na Bikira Maria katika safari yao takatifu nchini Misri, pamoja na hekalu la Kiyahudi – hali inayoifanya sehemu hiyo kuwa kielelezo cha kipekee cha mshikamano wa kidini.

Katika ziara hiyo, washiriki wa toleo la tano la Udhamini wa Nasser walipata fursa ya kutembelea kwa kina Msikiti wa Amr Ibn Al-As, pamoja na makanisa na nyumba za watawa zilizotembelewa na Kristo na Bikira Maria. Walipokea maelezo ya kina kuhusu urithi wa kihistoria wa Misri ya Kale, historia ya majengo hayo, alama na michoro ya kidini, pamoja na uhusiano wa kihistoria na wa kiroho baina ya dini tatu za mbinguni, unaoonekana kwa uwazi katika eneo hilo la kipekee. Washiriki wa Udhamini huo walieleza furaha yao kubwa na mshangao wao kutokana na ubunifu wa usanifu wa majengo ya kale ya Kimisri, na uzuri wa alama za kihistoria zinazoakisi ustaarabu mbalimbali uliopitia katika ardhi ya Misri. Walisifu sana mfano wa kipekee wa ushirikiano wa kidini unaojitokeza katika eneo la Mchanganyiko wa Dini, pamoja na alama na kazi za sanaa zinazoakisi roho ya uvumilivu, maelewano, na maisha ya pamoja kati ya dini tofauti.

Jukwaa la Nasser la Kimataifa: Warsha ya "Mabadilishano ya Kitamaduni" Yafunga Siku ya Kumi na Tano ya Udhamini wa Nasser kwa Uongozi  – Toleo la Tano

Katika taarifa yake ya mwisho kwa siku hiyo, Jukwaa la Nasser la Kimataifa lilitangaza kufungwa kwa shughuli za siku ya kumi na tano za toleo la tano la Udhamini wa  Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa  kwa kuandaa warsha maalumu iliyoangazia mada ya "Mabadilishano ya Kitamaduni". Warsha hiyo iliendeshwa na timu mahiri ya washauri na watoa mafunzo, walioteuliwa kutoka kwa wahitimu wa awamu mbalimbali za Udhamini wa Nasser na Shule ya Afrika 2063, ambao wana uzoefu mpana katika nyanja zao mbalimbali.

Miongoni mwa wawezeshaji wa warsha hiyo walikuwa: Dkt. Ahmed Mokhtar, mshauri wa sera za umma na utetezi katika Kituo cha Taarifa na Usaidizi wa Maamuzi katika Baraza la Utamaduni la Uingereza, na Mhitimu wa Kundi la pili la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi, na Dkt. Rajaa Magdy, Mhadhiri msaidizi katika Chuo Kikuu cha Ahram Canadian, Kitivo cha Famasia, na Mhitimu wa Kundi ya nne ya Udhamini, na Dkt. Bassem El-Maghraby, mhadhiri wa sayansi ya siasa na usimamizi wa umma katika Chuo Kikuu cha Suez Canal, na Mhitimu wa toleo la tatu, na Dkt. Rasha Hussein El-Sayed, mjumbe wa kiufundi katika ofisi ya Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, na mhitimu wa Shule ya Afrika 2063.

Warsha hiyo ilishuhudia ushiriki mkubwa kutoka kwa washiriki wa kimataifa waliokuwa na ari kubwa ya kubadilishana maarifa. Kila ujumbe wa vijana uliwasilisha mada maalum kuhusu utamaduni wa nchi yao, historia yake, mila na desturi, pamoja na vivutio vyake vya utalii, vyakula vya jadi, na alama zake za kitaifa. 

Mazungumzo yalijaa ari ya maelewano na kusisimua yaliyodhihirisha utofauti mkubwa wa tamaduni za washiriki na hali ya wazi ya kupokea tamaduni nyingine. Washiriki walibadilishana hadithi na maarifa kuhusu urithi usioonekana kama vile muziki, ngoma, hadithi za kale, na sanaa ya mavazi ya jamii zao, hali iliyotoa ladha ya kibinadamu na kimataifa kwenye warsha, na kuongeza thamani ya mazungumzo ya tamaduni mbalimbali.

Warsha ya “Mabadilishano ya Kitamaduni”, iliyohitimisha shughuli za siku ya kumi na tano za toleo la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, iliendelea kwa saa nyingi hadi usiku wa manane kutokana na hamasa kubwa na ushiriki hai wa washiriki. Vijana walionesha kuvutiwa sana na maudhui yaliyowasilishwa, huku wakieleza kuwa fursa hii ya kipekee imewasaidia kujifunza kwa karibu kuhusu tamaduni mbalimbali kutoka duniani kote. Washiriki walisisitiza kuwa warsha hii ni miongoni mwa kumbukumbu muhimu na zenye athari kubwa waliyoipata wakati wa ushiriki wao katika mfuko, kwani iliakisi maadili ya kuishi kwa pamoja, utofauti wa kitamaduni, na hali ya uwazi katika kuelewa wengine.

أخبار ذات صلة: