البحث

Ujumbe wa vijana washiriki wa kundi la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa watembelea Chuo cha Kijeshi cha Misri

2025/05/27

Jukwaa la Nasser la Kimataifa limetangaza katika taarifa yake leo Jumatano asubuhi kuhusu kuandaliwa kwa ziara ya Chuo cha Kijeshi cha Misri kwa ajili ya ujumbe wa vijana wanaoshiriki katika kundi la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, ikiwa ni sehemu ya shughuli za siku ya kumi na tatu za Udhamini huo unaofanyika chini ya Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi na kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa, kwa kushirikisha takriban vijana 150 wa kiume na wa kike kutoka mataifa mbalimbali duniani, wenye utaalamu tofauti wa kiutendaji, pamoja na baadhi ya vijana wenye ushawishi mkubwa katika jamii zao.

Viongozi wa Chuo cha Kijeshi cha Misri waliwapokea ujumbe wa vijana wanaoshiriki katika kundi la tano ya Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, kwa uwepo wa Meja Jenerali Ismail El-Far, Msaidizi Mkuu wa Waziri wa Vijana na Michezo anayeshughulikia masuala ya vijana na mahusiano ya serikali, pamoja na Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Jukwaa la Nasser la Kimataifa na Mkurugenzi wa Ofisi ya Vijana wa Kusini Duniani, pamoja na viongozi wengine kutoka chuo hicho na Wizara ya Vijana na Michezo.

Ziara ilianza kwa picha ya pamoja, ikafuatiwa na matembezi ya utangulizi ambapo washiriki wa kundi la tano la Udhamini huo walipata wasilisho lililoelezea historia ya kuanzishwa kwa Chuo cha Kijeshi cha Misri, maendeleo yake kwa miaka mingi, vyuo vilivyoko ndani yake, na nafasi yake ya kipekee katika kuandaa na kukuza vipaji vya kijeshi kwa viwango vya juu vya umahiri na nidhamu. Uwasilishaji huo pia ulielezea hatua mbalimbali ambazo chuo hicho kimepitia na programu za kielimu zinazotolewa. Baada ya hapo, washiriki walitembelea baadhi ya miundombinu ya chuo hicho, ikiwemo ukumbi wa mazoezi, uwanja wa squash, pamoja na vyumba vya malazi ya wanafunzi, na hivyo kupata nafasi ya kushuhudia kiwango cha juu cha vifaa vya kisasa vinavyopatikana kwa wanafunzi wa chuo hicho. Hii inaonesha wazi jinsi taasisi ya kijeshi inavyotoa mazingira ya kujifunzia yaliyo bora yanayochanganya taaluma, afya na maisha ya kila siku ili kuandaa viongozi bora kwa ajili ya kulitumikia taifa kwa ufanisi na weledi.

Mwisho wa ziara hiyo, washiriki wa kundi la tano ya udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa walitoa shukrani na pongezi zao za dhati kwa uongozi wa kisiasa na kwa jeshi la Misri kwa kuwaandalia ziara hizi muhimu zimezokuwa na athari kubwa chanya katika kuelewa uwezo mkubwa na wa kisasa wa jeshi la Misri. Washiriki hao walithibitisha kuwa kile walichokiona kuhusiana na nidhamu, maandalizi na miundombinu ya kisasa ni kielelezo cha kiwango cha juu cha utayari wa jeshi la Misri katika kulinda taifa na kulinda usalama wake. Pia walivutiwa sana na uzalendo na moyo wa kujitolea waliouona kwa wanajeshi wa Misri, wakisisitiza kuwa uzoefu huo umeongeza maarifa yao na kuwajaza fahari juu ya uwezo wa taifa la Misri kuendeleza maendeleo pamoja na kulinda usalama wake wa kitaifa.

Kwa upande wake, Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Jukwaa la Nasser la Kimataifa, alisema kuwa ziara ya ujumbe wa vijana wanaoshiriki katika kundi la tano la Udhamini huo katika Chuo cha Kijeshi cha Misri ni mojawapo ya vituo muhimu na vya kuhamasisha zaidi katika ratiba ya Udhamini. Ziara hiyo iliwapa washiriki fursa adimu ya kujionea kwa karibu mfumo wa mafunzo ya kijeshi ndani ya moja ya taasisi kongwe za kijeshi katika ukanda huu. Alisisitiza kuwa washiriki walionesha kuvutiwa sana na kiwango cha maandalizi na mpangilio, pamoja na uzalendo na nidhamu waliyoishuhudia chuoni hapo. Aliongeza kuwa ziara hiyo ni ujumbe wenye nguvu kwa vijana kuhusu umuhimu wa nidhamu, kazi ya kitaasisi, na nafasi ya taasisi za kijeshi katika ujenzi wa taifa la kisasa.

"Jukwaa la Nasser la Kimataifa": Ujumbe wa vijana wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa watembelea mgahawa wa Koshari Abu Tarek wakifurahia mandhari ya kijadi ya Kimisri

Jukwaa la Nasser la Kimataifa liliendelea kusema katika taarifa yake kuwa shughuli za siku ya kumi na tatu za kundi la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa zilihitimishwa kwa kuandaa ziara ya ujumbe wa vijana kwenda kwenye mgahawa maarufu wa "Koshari Abu Tarek".

Katika tukio linaloonyesha roho halisi ya ukarimu wa Kimisri, mgahawa wa "Koshari Abu Tarek" ulio katikati ya jiji la Kairo uliwapokea kwa furaha ujumbe wa vijana wa awamu ya tano ya Mpango wa Uongozi wa Nasser. Eneo hilo lilijawa na mandhari ya kijadi yenye furaha, likipambwa kwa miziki ya kitamaduni ya Misri na sauti ya “mizmar baladi” iliyotawala tukio hilo, ikiweka mazingira ya sherehe ya kipekee yaliyovutia macho ya kila mtu. Tabasamu zilikuwa zimejawa usoni mwa waliohudhuria, huku maeneo ya mgahawa yakiwa yamepambwa kwa mapambo ya kitamaduni yanayoakisi roho ya Kairo ya zamani, jambo ambalo liliunda hali ya furaha ya pamoja. Mapokezi ya ujumbe wa vijana yamekuwa ishara ya kweli ya maadili ya Kimisri katika ukarimu na kupokea tamaduni mbalimbali.

Ziara Yageuka Kuwa Maonesho ya Utamaduni wa Kimisri Katikati ya Jiji la Kairo

Ziara hiyo iligeuka kuwa kama onyesho dogo la kitamaduni, ambapo wafanyakazi wa mgahawa walijipanga pande zote za lango kuu, wakiwapokea wageni kwa midundo ya nyimbo za kitamaduni zilizotawala anga. Baadhi yao walivaa mavazi ya kifolklore yanayoakisi urithi wa watu wa Misri, na hivyo kuongeza mvuto wa kuona kwenye mandhari ya sherehe hiyo. Wageni walipandisha bendera za nchi zao katika tukio lililoonesha utofauti na udugu kati ya mataifa, huku raia na wapita njia wakishiriki kwa shauku kubwa, wakifurahia tukio hilo pamoja na wageni, jambo lililogeuza ziara hiyo kuwa hafla ya mawasiliano ya kitamaduni na kibinadamu kati ya vijana wa dunia nzima katika moyo wa mji mkuu wa Misri.

Washiriki wakundi la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, ambao wanatoka katika nchi mbalimbali za Afrika, Asia, na Amerika ya Kilatini, walieleza furaha yao kubwa kutokana na uzoefu huu wa kipekee uliounganisha tamaduni na ukarimu wa Kimisri kwa namna ya kipekee kabisa. Walisifu hali ya ukarimu na joto la mapokezi waliyopewa na wananchi wa Misri, wakisisitiza kwamba ziara yao katika mgahawa wa “Koshari Abu Tarek” haikuwa tu burudani bali ilikuwa ni tukio la kibinadamu na kitamaduni lililodhihirisha kiini cha asili na ukarimu wa jamii ya Kimisri. Washiriki wengi walithibitisha kuwa mwingiliano wa moja kwa moja na wananchi wa Misri katika mazingira haya ya kitamaduni yenye uhai umeunda hisia za kipekee ambazo zitabaki katika kumbukumbu zao. Pia walieleza kuwa mipango kama hii huimarisha maadili ya mazungumzo na kuelewana kati ya watu, na kuchangia kujenga madaraja ya maelewano na ushirikiano, hasa miongoni mwa vijana, jambo linalosaidia kudumisha amani na maendeleo endelevu duniani kote.

أخبار ذات صلة: